DAKTARI DARAJA LA II (MEDICAL OFFICER GRADE II)-492 Posts

Admin
Tanzania
Posted on Feb 14, 2026

Job Description

1. Kufanya kazi zote za matibabu hospitalini zinazohusiana na magonjwa mbalimbali yakiwemo magonjwa ya watoto, magonjwa ya akina mama na upasuaji wa kawaida na wa dharura.
2. Kutoa na kusimamia elimu ya afya pamoja na kuboresha afya ya jamii katika Wilaya na Mikoa au eneo lake la kazi.
3. Kuchunguza, kufuatilia na kuzuia milipuko ya magonjwa.
4. Kutunza takwimu na kuzitumia kama inavyoelekezwa katika misingi ya MTUHA.
5. Kupanga na kutathimini huduma za afya katika eneo lake la kazi.
6. Kufundisha wanafunzi na watumishi waliopo kwenye eneo la kazi.
7. Kusimamia na kuelekeza wafanyakazi walio chini yake.
8. Kubuni na kuendesha utafiti na kusambaza matokeo.
9. Kubuni na kutayarisha mikakati ya kuinua ubora wa huduma ya fani yake.
10. Kuandaa mipango na makisio ya bajeti ya huduma za afya.
11. Kushiriki, kuhakiki na kuboresha huduma za afya (medical audit and quality improvement).

Application Period
13/02/2026 - 27/02/2026

Qualifications

Kuajiriwa wenye Shahada ya Udaktari kutoka Vyuo Vikuu/Vyuo vinavyotambuliwa na Serikali waliomaliza “Internship” na kupata usajili kutoka Baraza la Madaktari Tanganyika (Medical Council of Tanganyika).

Want to apply for this position?

Please sign in or create an account to apply for this job.